Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la habari la ABNA, gazeti la Kiebrania la “Israel Hayom” lilikiri kwamba vita dhidi ya Irani vimalizika kwa kushindwa kwa kimkakati kwa utawala wa Kizayuni. Mfumo unaotawala nchi hii bado upo imara, na ina urani iliyorutubishwa.
Katika muendelezo wa ripoti hii imeelezwa: Utawala wa Kizayuni haukuweza kutimiza malengo yake ya kimkakati katika vita dhidi ya Irani na ulitoka kwenye vita hivi dhaifu zaidi kuliko hapo awali. Hii ni kinyume na Irani ambayo, licha ya kupata mapigo makubwa, imetoka kwenye vita ikiwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali.
Kwa mujibu wa ripoti hii, bunge la utawala wa Kizayuni linajishughulisha na michezo ya kisiasa na liko mbali kabisa na mchakato wa makubaliano na Irani. Katika eneo la kaskazini, mashambulizi yanaendelea pia. Kila siku inazidi kuwa wazi kwamba maneno ya maafisa wa Kizayuni kuhusu uhuru wa kutenda dhidi ya Hezbollah ni matupu.
Your Comment